Posts

Showing posts from January, 2018

Mbunge ahofia uhaba wa wataalamu sekta ya afya nchini

Na, Mwandishi Maalum Sauti ya Mnyonge, Dodoma MBUNGE wa Hanang Dk.Mery Nagu (CCM) ameonesha kuwa na wasiwasi kuwa kuna uwezekano wa viongozi kuhamasisha ujenzi wa vituo vya afya pamoja na zahanati lakini wasiwepo wataalamu wa sekta ya afya kutokana na kutokuwepo kwa watumishi wa kutosha. Akiuliza swali jana bungeni Dk.Nagu aliitaka Serikali ieleze ina mikakati gani ya kuongeza watumishi wa sekta ya afya katika vituo mbalimbali vya afya na zahanati kutokana na kukosekana kwa wataalam. “Je si kazi bure kama wananchi watajenga vituo vya Umma vya afya na zahanati lakini havitumiki je serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika vituo hivyo licha ya kuwepo kwa upungufu mkubwa wa watumishi katika sekta hiyo” alihoji Dk.Nagu. Awali katika swali la msingi la mbunge wa Busanda Lolensia Bukwimba (CCM) alitaka kujua serikali ina mkakati gani wa kuondoa uhaba wa watumishi wa sekta ya afya katika mkoa wa Geita kutokana na tatizo hilo kuwa kubwa. “Tatizo la uhaba wa watumishi katika sekta y

SERIKALI: hata sarafu za zamani bado ni halali na zinatumika

Na, Mwandishi Maalum Sauti ya Mnyonge, Dodoma IMEELEZWA kuwa  sarafu zote zilizowahi kutolewa na Benki Kuu Tanzania(BOT) tangu mwaka 1966 bado ni halali kwa matumizi nchini na zinatumika kwenye miamala ambayo si ya fedha taslimu. Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kuteuliwa Salma Kikwete (CCM). Mama Salama Katika swali lake alisema vijana waliozaliwa  kuanzia miaka ya 1990 na kuendelea hawazijui sarafu za senti 5, 10, 20, 50,.  “Kwanini serikali haioni ni wakati muafaka sasa kurudisha sarafu hizo kwenye mzunguko ili vijana wengi waweze kuzijua” alisema.. Dk.Ashantu alisema alisema BoT imepewa kisheria jukumu la kuzalisha fedha za noti na sarafu kulingana na mahitaji na mazingira ya kiuchumi yaliyopo. Alitaja mambo muhimu yanayozingatiwa wakati wa kuondoa na kuingiza katika soko noti na sarafu ya thamani ndogo na kubwa ni mfumuko wa bei wa bidhaa za huduma, kulinda thamani ya shilingi na wepesi wa s

TRA yakusanya bilioni 16.7 katika majengo

Na, Mwandishi Maalum Sauti ya Mnyonge, Dodoma MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya jumla ya sh. Bilioni 16.7 ikiwa ni kaodi ya majengo mbalimbali. Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni na Naibu Waziri wa Fedha Dk. Ashatu Kijaji alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kavuu  Dk.Prudenciana Kikwembe (CCM) Dk.Ashatu alisema kwa mujibu wa Sheria ya fedha ya mwaka 2017 kifungu cha 64 kimebainisha kuwa TRA itakusanya kodi za majengo. Alisema ukusanyaji huo utafanyika katika Majiji, Miji na Miji midogo yote nchini badala ya Mamlaka za serikali za Mitaa. Naibu Waziri alisema kwa kuwa majengo mengi hayajafanyiwa uthamini Serikali kupitia Bunge lilifanya uamuzi wa kuweka kiwango maalum cha kulipa. Alisema kiwango hicho ni Sh.10,000 kwa majengo ya kawaida n ash. 50,000 kwa majengo ya ghorofa. “Viwango hivi ni vya mpito wakati serikali inakamilisha zoezi la uthamini kwa majengo yote yanayostahili kulipiwa kodi ya majengo. Alisema majengo yote yaliyofanyiwa uthamini yanalipiwa viwango stahiki kulin

Serikali kujenga kituo kikubwa kutibu "mateja" mjini Dodoma

Na, Mwandishi Maalum Sauti ya Mnyonge, Dodoma SERIKALI imepanga kuanzisha kituo kikubwa cha kuwapatia tiba waathirika wa dawa za kulevya kwa njia ya kazi kituo kitajengwa Mkoani Dodoma. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi Ajira naVijana,Antony Mavunde alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kiembesamaki Ibrahim Mohamed  Raza (CCM) Katika swali lake Raza alitaka kujua  ni lini serikali itachukua hatua kwa kuwasaidia vijana walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya . Mavunde alisema serikali inatambua tatizo la matumizi ya dawa za kulevya na athari zake kwa vijana . Alisema katika kukabiliana na hilo Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imekuwa ikichukua hatua kadhaa kuwasaidia vijana hao . Alisema moja ya hatua ni pamoja na kutoa tiba kwa waathirika ambapo hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana jumla ya vituo vitano vya tiba ya methadone vilisha anzishwa. Mavunde alisema vilianzishwa katika Hospitali ya Muhimbili, Temeke, Mwananyamala, Zanzibar na Mbeya. Alisema kupitia vituo

Wamiliki bodaboda watakiwa kuwapa mikataba wanaowaajiri kuziendesha, na kutakiwa kuzikatia bima kubwa

Na, Mwandishi Maalum Sauti ya Mnyonge, Dodoma WAAJIRI nchini wanaotoa ajira kwa vijana waendesha pikipiki au bajaji wametakiwa  kuzingatia sheria ikiwa ni pamoja na kuwa na mikataba. Hayo yalisemwa jana bungeni na  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi Ajira na Vijana Anthony Mavunde alipokuwa akijibu swali. Mavunde alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Uzini  Salum Mwinyi Rehani (CCM) aliyetaka kujua ni lini serikali itawatambua rasmi dereva wa bodaboda  au bajaji kwa kuwaandikia mikataba na kuwawekea akiba  na kulipiwa mifuko ya Hifadhi ya jamiii. Mavunde alisema kuwa mbali na mikataba pia waajiri hao wanatakiwa kuhakiokisha waajioriwa wao wanapata huduma zingine muhimu zinazowawezesha kufanya shughuli zao kwa ufanizi na kwa kuzingatia usalama wa uhai wao na vyombo vyao. Alisema serikali itaendelea kusimamia matakwa ya sheria yanayomtaka mwajiri kutoa mikataba hiyo ikizingatiwa kwamba mkataba unabeba haki za msingi na wajibu kwa kila upande. “Nichukue fursa hii kutoa maagizo kwa waaji

Walimu watakiwa wasitumie wabunge kuomba uhamisho

Na, Mwandishi Maalum Sauti ya Mnyonge, Dodoma WALIMU pamoja na watumishi wengine wametakiwa kuacha mara moja kutumia viongozi wakiwemo wabunge kuwaombea uhamisho wa vituo vya kazi. Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Joseph Kakunda alipokuwa akijibu swali la Rehema Migill Viti Maalum CUF Kakunda alisema serikali inatambua kwamba uhamisho wa watumishi wa umma ni haki ya mtumishi endapo atazingatia utaratibu uliowekwa . Alisema kuanzia Julai 2017 hadi sasa, serikali imetoa vibali vya uhamisho kwa walimu 2,755. Naibu huyo alilieleza Bunge kuwa taratibu za kutoa vibali vya uhamisho kwa walimu wengine walioomba zinaendelea.  “Nachukua nafasi hii kuwaelekeza walimu pamoja na watumishi wengine wote, kuzingatia utaratibu na waache kutumia viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge kuwaombea uhamisho” alisema. Aidha Naibu Waziri alisema hakuna vikwazo kwa walimu wanaotaka kuhama vituo vyao vya kazi kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kufuata wenza wao au ugonjw

Wananchi Nyakatanga wasema sasa wana uhakika wa maisha

Image
Na, Mack Ngaiza Sauti ya Mnyonge, Kanda ya Ziwa Wananchi wa kata ya Nyakatanga wilayani Muleba, wamesema kuwa uhakika wa maisha yao yameanza kupata ufumbuzi kutokana na kujengewa zahanati baada ya kuishi kwa shida wakitembea zaidi ya kilomita10 kufuata huduma ya afya. Wametoa kauli hiyo na kuiomba serikali kuharakisha kutuma wauguzi kwenye zahanati hiyo, baada ya kutembelea ujenzi wa zahanati hiyo. Mkuu wa Mkoa wa Kagera,Mhe. Meja Jenerali MST Salum M. Kijuu leo tarehe 30/01/2018 ametembelea na kukagua shghuli za Ujenzi wa zahanati ya Nyakatanga iliyojengwa kwa ufadhili wa shirika la World Vision,mchango wa Mbunge Jimbo la Muleba Kaskazini Mhe. Charles Mwijage (Waziri wa Viwanda, Uwekezaji na Biashara) na nguvu ya jamii. Mradi huu umegharimu kiasi cha Tsh. 56,761,100 kati ya hizo, World Vision imechangia kiasi cha Tsh 47,000,000.00 Mbunge wa jimbo la Muleba Kaskazini, Mhe. Charles Mwijage amechangia Tsh. 5,451,000.00 na wananchi wamechangia kiasi cha Tsh. 4,310,000.  Uongozi wa kata un

Soma kilio cha maumivu ya kisaikolojia anacholia mama huyu aliyebakwa

Image
Na, Shirazy Haroub Sauti ya Mnyonge, Pemba MWANANMKE mmoja (30) mkaazi wa Kiungoni  Wete Pemba, anaendelea kuteseka kiakili  na kimwili,  baada ya kudai kuwa amebakwa na kunajisiwa na kijana aliemtaja kwa jina la Mohamed Omar Khamis, ambae ni  mtoto wa sheha wa shehia ya Kiungoni wilayani humo. Picha ya Mtandaoni, ikimuonyesha mwanamke anayedondokwa na chozi Akizungumza kwa huzuni  huko nyumbani kwao Kiungoni mwanamke huyo alisema,  tukio hilo lilitokea kipindi cha nyuma, ambapo alikutwa na mkasa huo, alipokwenda porini kutafuta kuni, ndipo ghafla alimuona kinana huyo na kuanza kumfuata nyuma huku akiwambia kuwa anataka kufanyanae mapenzi. “Alikua ananiuliza, kwa sauti ya chini juu ya kutaka kufanya mapenzi na mimi ingawa nilikuwa nakataa na kuanza kumkimbi kimbia, lakini  mwisho akanivamia ghafla na kisha na kuniangusha chini'', alisema mweanamke huyo.  Alifafanua kuwa, baada ya kufanyiwa tukio hilo alikurupuka na kwenda  mbio, ingawa kumbe kulikua na mwenzake aliyemtaja kuwa

Wanyonge wahimizwa kuwapatia watoto malezi pa pamoja kumaliza ulawiti na ubakaji

Image
Imeandaliwa na Zuhura Juma Sauti ya Mnyonge, Pemba KWA miaka mingi Zanzibar ilisifika kuwa ni visiwa vilivyoheshimika, kwa watu wake kuwa waungwana, wema, karimu na waliokuwa na ihsani iliyotukuka. Watu wake, hasa majirani, waliishi kama ndugu na kusaidiana kwa shida, msiba na furaha katika malezi ya watoto.  Kila mzazi alimuona mtoto wa mwenzake kama ni wake, na aliyekuwa hana mapenzi ya watoto alionekana mtu wa ajabu na haeleweki. WARATIBU wa wanawake na watoto wa shehia za Mchanga mdogo, Kiungoni, Mjini ole, Kangagani, Shengejuu na Kinyikani wilaya ya Wete Pemba, pamoja na wadau wengine wakiwa katika mkutano, wa kupinga vitendo vya udhalilishaji katika jamii na namna gani vinaweza kuondoka Kwa bahati mbaya, visiwa hivi katika miaka ya karibuni vimeanza kupoteza sifa hizo na watu wengi wanaamini hii inatokana zaidi na kukosekana malezi bora ya pamoja. Hali hii, ilielezwa vizuri na bibi kizee mmoja kwa kusema, ilikuwa kawaida wakati wa ujana wake kama hakumuona mwanawe nyumbani, baad

Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar na harakati za kupambana na rushwa

Image
Na Haji Nassor Sauti ya Mnyonge, Zanzibar AZMA moja ya Mapinduzi ya Zanzibar, yalioasisiwa mwaka 1964, na jemedari wa Mapinduzi hayo, na rais wa kwanza wa Zanzibar marehemu Amani Abeid Karume, ilikuwa kuondoa ujinga, maradhi na rushwa. Sasa ni miaka 54, ya Mapinduzi ya Zanzibar tokea, jemedari huyo kutukomboa sisi wazanzibari, katika mikono ya wanyonyaji na wakandamizaji waliokuwa wakila matunda ya wazalendo . Aliwahi kusema kuwa“ leo wananchi sasa tuko huru, lazima tupambane na maradhi, ujinga na rushwa, maana hawa ndio adui wa haki” ni matamshi yake kati ya moja ya hutuba zake, akiwahutubia wanajeshi . Kumbe wazo, fikira, busara na nia ya kuwakomboa wananchi wa Zanzibar na rushwa, kwa kiongozi huyu na rais wetu wa kwanza wa rais, ilianza zamani na leo ni miaka 54 sasa. Maana kihistoria hata mtawala wa Zanzibar aliekuwepo ndani ya mwaka 1934 , alionekana kijibabaisha, kuwa eti anapamba na rushwa, wakati akiwakandamiza wazalendo. Kwenye sheria Adhabu “Pin decree’ cap no 13 ya mwaka 193

Mkuu wa Mkoa atoa miezi mitatu wananchi kujisajili daftari la wakazi

Image
Na, Florence Sanawa Sauti ya Mnyonge, Mtwara MKUU wa Mkoa wa Mtwara Gellasius Byakanwa ameagiza ndani ya miezi mitatu kwa wananchi wa mkoa huo kujiandikisha katika daftari la makazi. Akizindua daftari hilo jana alisema kuwa ili kuimalisha ulinzi na usalama wa mkoa wanannchi wanapaswa kujiandikisha katika kipindi hicho bila kukosa. Alisema kuwa andikishwaji wa daftari hilo utasaidia kutatua masuala ya kiharifu yanayotokea katika mitaa yetu hivyo wananchi wanapaswa kufahamiana ili kudumisha amani ya mkoa. “Hili zoezi hilo sio la kupoteza muda kutokana na umuhimu wa usalama na maendeleo ya nchi, ili serikali iweze kutusaidia lazima ijue idadi yetu hapo ndio bajeti inaweza kupangwa kulingana na idadi ya watu na mahitaji yaliyopo ndani ya jamii hatutaweza kuondoka katika umasikini bila kujua idadi yetu…… “Daftari hili limeandaliwa tangu 2011 halijawahi kutumika hata wakuu wa mikoa waliotangulia hakuwahi kujiandikisha wala kujua mwenyekiti wao wa mtaa ninani ndio maana nitoa miezi mitatu kwa

Uendeshaji shule wakwama baada ya wajumbe wa bodi kususia vikao "visivyo na kitu"

Image
Na, Florence Sanawa Sauti ya Mnyonge, Mtwara WAJUMBE wa bodi za shule mkoani Mtwara wamesusia kuhudhuria vikao vya uendeshaji wa shule kutokana na kutolipwa posho baada ya serikali kutangaza dhana ya elimu bila malipo.  Shirika la faidika wote kwa pamoja (FAWOPA) lilibaini hali hiyo wakati wa mradi wa ufuatiliaji wa matumizi ya rasirimali za umma katika sekta ya elimu manispaa ya mtwara mikindani kutoka kutembelea shule mbalimbali na kubaini kusimama kwa maamuzi mengi.  Akizungumza katika kikao cha wadau wa elimu kilichoandaliwa na shirika la faidika wote kwa pamoja (FAWOPA) ambapo maafisa watendaji kata, walimu wakuu, wachumi, wazazi na maafisa elimu walihudhuria, Mratibu wa shirika hilo Baltazar komba alisema kuwa vikao vingi vilisimama baada ya serikali kutoa agizo la elimu bure. Alisema kuwa kukwama kutokana na kutokuwepo kwa michango shuleni hivyo wajumbe hao kukosa posho ya kujikimu hali ambayo inawafanya walimu wachukue maamuzi wenyewe. “Hivi vikao vya bodi za shule visipo endel

Mkuu wa Wilaya aagiza TAKUKURU kuchunguza mapato mgodi wa dhahabu wa Kitunda

Image
Na Mwandishi Wetu Sauti ya Mnyonge, Sikonge MKUU wa wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora Peresi Magiri ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani humo kwenda kuchunguza upotevu wa mapato ya mgodi wa dhahabu Kitunda ili wahusika wote wawajibishwe. Amelitoa agizo hilo jana kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo baada ya madiwani kutoridhishwa na makusanyo ya ushuru wa mgodi huo na kulalamikia uwepo wa mianya mingi ya upotevu wa mapato hayo. Alisema lisemwalo lipo, haiingii akilini mapato ya mgodi wa dhahabu Kitunda yawe kiduchu kiasi hicho, kuna kitu hapa, ni lazima uchunguzi wa kina ufanyike ili kubaini fedha hizo zinaenda wapi na wahusika ni akina nani na hatua zichukuliwe. ‘Nimesikia malalamiko ya madiwani, naagiza uchunguzi wa haraka na wa kina ufanyike pale mgodini, TAKUKURU nenda kafanye hiyo kazi, na unipe taarifa haraka ili tuchukue hatua kwa watakaobainika’, alisema. DC alibainisha kuwa suala la ukusanyaji mapato sio la DC au DED pekee yake

Soma namna watoto wa wanyonge wanavyosomea chini ya mti mkoani Mtwara

Image
Na, Florence Sanawa Sauti ya Mnyonge, Mtwara WANAFUNZI wanyonge zaidi ya 200 wasomea chini ya mkorosho baada ya  madarasa yao yaliyojengwa kwa udogo kubomolewa  hali ambayo imewalazimu kusomea chini ya miti huku wakihofia kung’atwa na siafu miguu. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Omary Kipanga ameagiza madarasa hayo kubomolewa haraka huku wanafunzi hao wakianza kusomea chini ya miti ya mikorosho. Akizungumzia hali hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Kipanga alisema kuwa majengo hayo yalijengwa kwa utashi wa wananchi bila kushirikisha halmashauri hiyo. “Kile kilichokuwa kimejengwa sio kwa maagizo ya ofisi yangu mimi nilipita mwezi wa kumi shule zote kukagua lakini sikuona majengo kama yale kama ni kujenga wamejenga wananchi tena kama sio Novemba itakuwa Desemba……. “Hata mwongozo wa wizara ya elimu hausemi tujenge darasa kama lile hata jiko hatukuambiwa tujenge mfano ule hatukuagiziwa yale sio madarasa hata ingekuwa ya muda yale sio madarasa ule ni uchafu ulipo sio mahala pake nd

Waliotubu kutengeneza mkaa, wataka wenzao wanaoendelea wadhibitiwe

Na Haji Nassor Sauti ya Mnyonge, Pemba VIJANA kisiwani Pemba, walioamua kuachana na kazi ya upigaji mkaa, wameiomba wizara husika, kuwashughulikia vijana kutoka Tanzania bara, wanaoshirikiana na wenyeji, kuendelea na kazi hiyo kwa kasi. Walisema, wao wameshakubali kuacha na kazi hiyo, hasa kwa vile athari yake ni ya muda mrefu inayotokana na ukataji miti, ingawa wapo wengine, wakishirikiana na wageni wakifanya kazi hiyo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, walisema kisiwa cha Pemba, kimekuwa kikipoteza miti kadhaa siku hadi siku, kutokana na ukataji hasa kwenye sekta ya utengenezaji mkaa. Walisema lazima wizara husika, iingilie kati juu ya vijana hao, ili kuwadhibiti kwa lengo la kukinusuru kisiwa cha Pemba na upotevu wa mkubwa wa miti. Mmoja kati ya vijana hao, Ali Mkubwa Hussein, alisema wao wameshaachana na kazi hiyo na kuelekea kwenye kilimo cha mboga mboga, na hasa baada ya kuelimishwa juu ya athari za ukataji miti. “Sisi tuliitwa kwenye semina na kuelezw

Wataka minada ya korosho kusitishwa kufuatia bei kushuka

Image
Na, Marry Sanyiwa Sauti ya Mnyonge, Mtwara Wakulima wa korosho wa wilaya ya Tandahimba na Newala Mkaoni Mtwara,wakifungua sanduku la tenda katika mnada wa kumi na mmoja ambao ulifanyika katika kijiji cha  kitama ya kwanza wilayani humo. Wakulima wa zao la Korosho wa wilaya ya Tandahimba na Newala Mkoani Mtwara, wameishinikiza Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) kusitisha kuendelea kwa minada ya korosho ghafi kutokana na bei ya zao hilo kuanza kushuka. Akizungumza katika mnada wa Kumi na moja uliofanyika katika kijiji cha kitama ya kwanza wilayani tandahimba  Mkulima wa zao hilo Selemani Chiwinde  anasema kwa sasa wanunuzi wamepungua kwa kiasi kikubwa hivyo hawezi kuleta ushindani wa soko katika zao hilo wakati minada inaanza. Alisema kuwa bei za minada imekuwa ikishuka siku hadi siku hadi kutoka bei juu ya shilingi 4128 hadi kufikia bei chini shilingi elfu 3400 hali ambayo inawatia hofu wakulima. “tunaiomba Bodi ya korosho wafanye mnada huu kuwa wa mwisho kwa sababu yanayojitokeza kwa sasa 

Vyoo vipya vyavutia wanafunzi kuhudhuria masomo

Image
Na Florence Sanawa Sauti ya Myonge, Mtwara UJENZI wa vyoo vipya katika Shule ya Msingi Madimba umeongeza hamasa kwa wanafunzi wa shule hiyo kuhudhuria masomo darasani hivyo kupunguza tatizo la utoro shuleni hapo.  Akizungumza wakati akipokea matundu 8 ya vyoo kutoka TPDC Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Madimba Hamis Nambunga utoro huo ulitokana na uhaba wa vyoo uliokuwepo shuleni hapo.  Alisema kuwa watoto wengi hasa wenye matatizo mbalimbali walishindwa kuhudhuria masomo na kufanya utoro uwe mkubwa kwakuwa walikosa mahali pa kujihifadhi kutokana na vyoo vya shule hiyo kutokuwa na mazingira ya kuridhisha.   Nambunga alisema kuwa baada ya shirika hilo kuwajengea matundu 8 sawa na asilimia 48 pekee wanaomba serikali na wadau wengine waweze kujitokeza ili kuweza kuboresha mazingira vyoo shuleni hapo ambapo hivi sasa matundu 10 ndio yanahitajika.  “Hali ilikuwa mbaya ilifkikia wakati serikali ilitaka kufunga shule yetu kutokana na tatizo la choo ujenzi wa hule hii utaongeza hamasa ya wazazi n