Posts

Showing posts from February, 2018

Kiwango kidogo cha ufaulu wa mitihani chamtia wasi wasi mkuu wa mkoa

Image
MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba, Hemed Suleiman Abdall amesema, amekiri kutoamini sababu ya wilaya ya Mkoani kutofanya vyema kwenye mitihani ya taifa kwamba   kumechangiwa na uhaba wa waalimu, bali ana mashaka na hamu na ari ya ufundishaji wa baadhi ya waalimu hao. Alisema anashangaa kuona baadhi ya skuli kama Mizingani sekondari na nyengine pana masomo hayana waalimu, ingawa ufuaulu wake ni mkubwa ukilinganishwa na yale masomo kama ya dini, Kiswahili na kiarabu ambayo yanawaalimu wa kutosha lakini ufaulu wake ni mbovu, Mkuu huyo wa Mkoa, ameeleza hayo skuli ya Mohamed Juma Pindua, alipokuwa akizungumza na waalimu wakuu, wa msingi, sekondari na wenyeviti wa kamati zao, kwenye mkutano wa kutathimi, kufuatia wilaya hiyo kutofanya vyema kwenye mitihani ya taifa iliopita. Alisema, yeye binafsi anamashaka na aria na hamu ya waalimu iwapo wanajua wanchokifanya wanapokuwa  madarasani bali kuna jambo jengine, ambalo lilisababisha ubovu wa matokeo hayo ya taifa na sio uhaba wa waalimu pekee. Mhe

Agizo la rais kwa wanyonge 177 wa Ngomeni Pemba laanza kutekelezwa

Image
WASTANI wa wananchi 177 wa kijiji cha Ngomeni shehia ya Mgelema wilaya ya Chakechake Pemba, wanaendelea kutengenezewa barabara yao kwa kiwango cha lami, ikiwa ni agizo maalumu la rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein. Wananchi hao awali, walitoa kilio chao cha ukosefu wa barabara ya kisasa, mbele ya rais wa Zanzibar wakati alipowatembelea mwaka jana, ndipo alipoitaka wizara husika, kuhakikisha wanaitengeneza ili iweze kupitika kipindi chote. Baada ya wizara kukamilisha hatua hiyo, wananchi hao walimuomba tena rais huyo wa Zanzibar, sasa kuwajengewa kwa kiwango cha lami, ambapo tayari ujenzi huo umeshaanza na kabla ya kumalizika kwa mwezi Machi mwaka huu, itakuwa imeshakamilika.   Ujenzi huo unaofanywa na Wizara ya Ujenzi, Miundombinu na Usafirishaji Zanzibar, kwa kiwango cha lami, umaenza miezi mitatu iliopita, na unatarajiwa kukamilika wakati wowote kabla ya mwisho wa mwezi ujao. Mhandishi ujenzi wa wizara hiyo, Khamis Massoud, alisema hatua

Serikali yabaini fedha za wanyonge kuishia mikononi mwa wabadhirifu

Image
WAZIRI Mkuu Kassimu Majaliwa amesikitishwa na matumizi maabaya ya fedha za mapato ya ndani yanayokusanywa kwa wanyonge kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo, badala yake kupelekwa wenye miradi mikubwa ambayo imetengewa fedha za serikali. Matumizi hayo mabaya yametokana na watumishi wa wawili wa Mji Masasi  ambao walishiriki kufuja fedha za mradi wa jengo la utawala zaidi ya milioni 1.8 ambazo zililetwa na serikali kutumiwa hali ambayo inmepelekea watumisihi hao kuchukuliwa na  kamanda wa taasisi ya kupambana na rushwa (PCCB)kwa mahojiano. Mahojiano hayo yatamuhusisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Fortunatus Kagoro ili aweze kutolea majibu fedha hizo. Alisema kuwa fedha hizo zinazotolewa katika miradi maalumu zinapaswa kutumika ipasavyo kwa kuisimamia kodi ya watanzania ili irudi katikamaendeleo. “Haya ndio mambo ambayo hatuvumilii Kamanda PCCB muite  aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri fortunatus kagoro atwambie mtiririko wa fedha hizo ziko wapi na hatumishi hao wakiwa nj

Kaya zaidi ya elfu tatu hatarini kwa magonjwa ya mlipuko Kagera

Image
Kaya 4,364, zipo hatarini kukumbwa na magonjwa ya milipuko wilayani Misenyi mkoani Kagera, kutokana na kutokuwa na vyoo na kuvitumia. Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi Bw. LIMBE BENARD,   wakati akizungumza na mwandishi wa mtandao huu juu ya mkakati kwa kaya zisizo na vyoo, ilhali zina mahitaji ya miundombinu hiyo muhimu. Amesema kuwa   takwimu hizo zimebainika katika mchakato wa kutambua vyoo bora kila kaya, uliofanyika katika mwezi January mwaka huu 2018, kwa kuhusisha jumla ya kaya 37,685 zilizokaguliwa na kuhojiwa kwa wanakaya wenyewe. Bw. LIMBE ameongeza kuwa katika utambuzi hu, zipo kaya ambazo zimekubali na kuanza uchimbaji na ujenzi wa vyoo, ingawa kaya 102 kati ya hizo zimekaidi kufanya hivyo, na kuilazimu serikali kuzitoza faini ya jumla ya shilingi laki 6 na elfu 50. Pamoja na kutozwa faini hizo, imeelezwa kuwa wanaendelea kufatiliwa kwa lengo la kujihakikishia kama wametekeleza agizo ili kuepusha kuwasababishia wengine matatizo ya kiafya

Wadau wataka ZBC iwezeshwe kushindana kihabari na luninga zingine

Image
Na, Haji Nassor Sauti ya Mnyonge, Pemba WADAU wa habari kisiwani Pemba, wameishauri Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar, kuendelea kujipanga vyema, ili Shirika la Utangaazaji Zanzibar ZBC liwezea kuingia katika soko la ushindani wa kihabari. Walisema shirika hilo kupitia tv yake ya rangi, ililianza mwanzo barani Afrika kwenye mwaka 1973, lakini linashindwa kwenda sambamba na vyombo vyengine ya habari, na kupoteza watazamaji. Wakizungumza kwenye mkutano wa kutafuta maoni kwa wadau juu ya kuimarisha utendaji wa kazi kwa vyombo vya habari ya serikali, uliofanyika uwanja wa michezo wa Gombani Chake chake kisiwani humo, walisema bado shirika hilo linamtihani mitambo yake. Walisema ni aibu kwa sasa kuona shirika hilo la utangazaji kupitia tv, vipindi na matangaazo yake yatabia ya kukata kata na wakati na mwengine kuzima kabisa na kuwakosesha raha watazamaji wake. Mmoja kati washiriki wa mkutano huo, sheha wa shehia ya Mkoroshoni Khamis Iddi Songoro, alisema yeye hujipanga

Pemba Kusini watakiwa kuharakisha hukumu

Image
Na Zuhura Juma, Sauti ya Mnyonge, Pemba MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba, Hemed Suleiman Abdalla, amewataka watendaji wa mahakama kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kusikiliza na kuzitolea hukumu kesi kwa muda mfupi zaidi, ili kuondosha usumbufu kwa wananchi. Alisema ili kufanya shughuli zao za kimaendeleo, ni muhimu kwa mahakama kuharakisha kesi na kuzitolea maamuzi mapema, jambo ambalo halitoathiri shughuli za kimaendeleo za wananchi katika kujiwezesha kiuchumi. Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya sheria Zanzibar,zilizofanyika  katika uwanja wa Tenis Mjini Chake Chake, alisema Serikali itashirikiana na mahakama ili kuhakikisha haki inapatikama na kuimarisha uchumi wa nchi. “Mashauri yanapokaa muda mrefu mahakamani bila kupatiwa hukumu, inaweza kuathiri  uchumi, kwani shughuli za wananchi huzorotesha shughuli za wananchi kiuchumi”, alisema Mkuu huyo. Kwa upande wake, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar ,Abdul-hakim Ameir Issa, aliwataka majaji, mahakimu na makadhi watimiza wajibu wao sa

Kama baba anaweza kubaka mwanawe usalama wa watoto upo wapi?

Image
Imeandaliwa na Zuhura Jumaa Sauti ya Mnyonge, Pemba Kwa kawaida mtoto akiumia, anapoona ameonewa au akitaka kitu hukimbilia kwa mzazi au yule anayehisi yupo karibu naye. WARATIBU wa wanawake na watoto wa shehia sita za wilaya ya Wete, masheha pamoja na wadau wengine wakiwa  katika moja ya mkutano wa kupinga vitendo vya udhalilsihaji  dhidi ya wanawake na watoto, uliofanyika uwanja wa Gombani Ni kwa mzazi ndipo anapoamini upo usalama wake na kupata mahitaji yake na mzazi hutarajiwa kuonyesha malezi mazuri na kumpatia mtoto anachostahili. Lakini baadhi ya hao waliopewa utukufu uliotukuka wa kuitwa watoto wa Adam na Hawa (binaadamu) sifa hii ya utu haipo na hufanya mambo zaidi ya wanyama. Hali hii ndio iliopelekea mtu anayefanya ushenzi au ujahili wa aina moja au nyengne kuitwa mnyama. Hivi karibuni tumesikia mambo ya kinyama yakifanywa sehemu mbali mbali za Unguja na Pemba na baadhi ya matukio kuwashitua watu na hata kutoamini waliyoyasikia. Katika orodha ya mtukio ya aina hii ni lile la

Wananchi watakiwa kufika mahakamani kusaidia kutoa ushahidi

Image
Na Haji Nassor,  Sauti ya Mnyonge, Pemba MRAJISI wa mahakama kuu jimbo Pemba Hussein Makame Hussein MRAJISI wa Mahakama kuu jimbo Pemba, Hussein Makame Hussein, amesema ili mtenda kosa aweze kutiwa hatiani,  suala la jamii kufika mahakamani kutoa ushadi, ni moja ya njia ya kuishahiwisha mahakama kufikia hatua hiyo. Alisema sio kweli kuwa, mwenye uwezo wa kifedha ndie anaeshinda kesi, kama baadhi ya dhana za watu zilivyo, bali kila shauri linalofikishwa mahakamani, ushahidi ndio kigezo cha hukumu. Mrajisi huyo, alieleza hayo jana skuli ya ufundi Kengeja wilaya ya Mkoani, alipokuwa akizungumza na waalimu na wanafunzi wa skuli hiyo, akiwa na kamati yake ya maandalizi ya siku ya sheria Zanzibar. Alisema yanapofanyika matendo kama ya jinai au madai, mahakimu na majaji huwa hawapo, hivyo mashauri hayo yanapofikishwa mbele yao, wa kuyatolea  maelezo ni mashuhda, na kisha kuiachia mahakama kufanya uamuzi. Katika hatua nyengine, Mrajisi huyo ambae pia ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya

Polisi Zanzibar wamsaka mama aliyetelekeza kichanga benchi la wagonjwa hospitalini

Image
Na Haji Nassor,  Sauti ya Mnyonge, Pemba JESHI la Polisi Mkoa wa kusini Pemba, limesema linaendelea kuweka mitego ya aina mbali mbali, ili kumnasa mama mzazi aliemtelekeza mtoto wake mchanga wa siku moja, kwenye mvungu wa bao la kukalia ndani ya hospitali ya Chambani wilaya ya Mkoani wiki iliopita. Jeshi hilo limesema tayari limefanya uchunguuzi wa shehoa kadhaa kisiwani Pemba na hata kuwatumia baadhi ya masheha, ili kuulizia iwapo  kuna mzazi aliejifungua na kisha mtoto kutoonekana. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, Kamanda huyo wa Polisi mkoani humo Shehan Mohamed Shehan alisema, bado jeshi lake halijakata tamaa juu ya kumpata mama huyo, na ndio maana linaendelea na uchunguuzi. Alisema, wanaweka mitego kwenye vijiji, mitaa, shehia a wilaya mbali mbali, kwa lengo la kujua habari zake na akipatikana ,baada ya kuhojiwa atafikishwa mbele ya vyombo vya sheria kujibu shitaka lake. Hivyo, ameitaka jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi na wasisite kutoa taar

Wanasheria Pemba watembelea shule mbalimbali kuadhimisha siku ya sheria Zanzibar

Image
Picha na Maelezo, Haji Nassor Sauti ya Mnyonge, Pemba WANAFUNZI wa skuli ya Ufundi Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, wakifuatilia mkutano wa elimu ya sheria, iliotolewa na wanasheria mbali mbali waliofika skulini hapo, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za kuelekea siku ya sheria Zanzibar, kamati hiyo ilikuwa chini ya Mwenyekiti wake Mhe: Hussein Makame Hussein MRAJISI wa mahakamu kuu Jimbo Pemba, Mhe: Hussein Makame Hussein, akijibu masuali mbali mbali ya wanafunzi wa skuli ya Ufundi Kengeja, wakati Kamati ya maandalizi ya sherehe ya siku ya sheria Zanzibar, ilipofika skulini hapo, kutoa elimu ya sheria BAADHI ya watendaji wa mahakama kisiwani Pemba, wakifuatilia mkutano wa kutoa elimu ya sheria, kwa wanafunzi wa skuli ya ufundi Kengeja wilaya ya Mkoani MWANASHERIA wa serikali na Mwendesha Mashitaka kutoka ofisi ya DPP, Ali Haidar Mohamed akizungumza kwenye mkutano wa elimu ya sheria, kwa wanafunzi wa skuli ya Ufundi Kengeja, ambapo ni shamra shamra za kuelekea siku ya sheria Zanzibar HAK