Posts

Showing posts from December, 2017

DC Tandahimba aamua kukomalia mimba kwa wanafunzi

Image
Na Florence Sanawa Sauti ya Mnyonge, Mtwara KUFUATIA kuwepo kwa tatizo kubwa la ujauzito kwa shule za sekondari Wilayani Tandahimba ambapo katika ripoti ya mwaka 2017 imeonyesha kuwa zaidi ya wanafunzi 55 wameacha shule kutokana na tatizo hilo. Hali hiyo imeilazimu kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ikishirikiana Mkuu wa Wilaya hiyo Sebastian Waryoba kufanya msako ili kuwabaini wanafunzi hao shule wanazotoka na kuwafahamu wazazi wao ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa. Kauli hiyo ameitoa juzi wakati wa kikao cha ushauri cha halmashauri ya wilaya  hiyo (DCC) ambapo baada ya kutopokea taarifa ya elimu iliyosomwa na afisa elimu sekondari sostenes luhende alisema kuwa taarifa hiyo imemshtua hivyo kutaka kujua hatua zilizochukuliwa baada ya wanafunzi hao 55 kuacha shule kutokana na ujauzito. Alisema kuwa kulingana na taarifa hiyo alisema kuwa lazima hatua zichukuliwa haraka ili iwe fundisho kwa wengine hatua ambayo inaweza kupunguza tatizo la mimba wilayani humo. Waryoba alisema kuw

Waziri aziagiza tafiti zaidi ili kuongeza uzalishaji wa mbegu

Image
Na Florence Sanawa & Marry Sanyiwa Sauti ya Mnyonge, Kanda ya Kusini NAIBU Waziri wa Kilimo Dk Mary Mwanjelwa ameziagiza taasisi zinazojishughulisha na utafiti wa mbegu nchini kuongeza uzalishaji wa mbegu bora ili kukidhi mahitaji ya wakulima nchini.  Kauli hiyo ameitoa juzi wakati alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendelea ambapo alisema kuwa uzalishaji wa mbegu kwa wingi unaweza kuhamasisha wakulima kuongeza mazao zaidi.   Alisema kuwa taasisi zinazo fanya utafiti nchini zinapaswa kuongeza juhudi ili wakulima wanufuaike na tafiti hizo ambazo zimekuwa zikiwanufaisha wakulima wachache zaidi hivyo kuto nufaika na tatifi hizo hivyo kushindwa kuzalisha kwa tija.  Dk Mwanjelwa alisema kuwa endapo vituo vingi vya utafiti vitazalisha mbegu kwa tija vinaweza kuwasaidia wakulima wengi ambao wanaweza kupata mbegu hizo kwa urahisi hivyo kuongeza uzalishaji nchini.   “Zipo taasisi nyingi kwenye taasisi zingine za utafiti wa kilimo wajiongeze kama taasisi ya NALIENDELE wanavyofanya

MAMCU yaonya viongozi waweka mawe kwenye magunia ya korosho

Image
Na, Florence Sanawa,  Sauti ya Mnyonge, Mtwara Kuelekea mwishoni mwa msimu wa korosho Chama kikuu cha ushirika cha Masasi, Mtwara Cooperative Union MAMCU kimetoa onyo kali kwa vyama vya msingi kuacha udanganyifu unaofanywa wa kuweka mawe katika magunia ya korosho ili kuongeza uzito wa bidhaa hiyo. Kaimu Meneja wa Chama hicho Potency Rwiza ansema  kuwa udanganyifu huo unaweza kuharibu soko la korosho kwa misimu iliyobakia. Hofu hiyo imejitokeza katika chama cha msingi cha Umoja ni Nguvu kilichopo wilayani Masasi na kufanikiwa kukuta moja ya magunia yaliyojazwa katika chama hicho yakiwa yamewekewa mawe katikati.  “Suala hilo sio mara ya kwanza kujitokeza katika kipindi cha ununuzi wa zao hilo, ambapo msimu uliopita liliwahi kulalamikiwa na wanunuzi ndio maana tuliamua kufanya uchunguzi na kubaini hilo na pia tulikuta korosho na mawe zimechanganywa ndio maana tuliamua kuwachukulia hatua na kuwakabidhi katika vyombo vya ulinzi ili hatua zingine ziweze kuendelea” alisema Potency Kwa upande

Wananchi wataka eneo la barabara lililokatika lijengwe daraja

Image
Na Haji Nassor Sauti ya Mnyonge, Pemba MADEREVA na wananchi wanaotumia barabara ya Mkoani- Chakechake, wamesema wakati umefika wa wizara husika ya ujenzi wa barabara, kujenga daraja maalum eneo la Changaweni Mkoani, kufuatia kuharibika tene eneo ambalo lilijegwa hivi karibuni na wizara hiyo. Walisema, ishara zinaonyesha eneo hilo asili yake ni kuwepo kwa mto unaokatisha chini kwa chini, na ndio maana kila mvua zinaponyesha, hujitokeza uharibifu. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye eneo hilo, walisema wanashangaa kuona miezi mitatu, iliopita wizara husika ilitumia gharama kubwa kujenga eneo hilo, na tayari mvua ilionyesha juzi, pameshaharibika tena. Mwananchi Hamad Khamis, alisema awali juzi hiyo alipopita alishuhudia ufa mkubwa ulipakana na barabara kongwe, na baadae majira ya mchana alionona hali kuongezeka. “Hata sisi wapiti njia hii hali inatutia wasi wasi, maana hutujui wakati gani inaweza kukatika, na kila mtu na wa umri wote wanapita hapa, lazima pajengwe daraja”,alis

TAFITI: Pembejeo za bure hazikunufaisha wakulima wa korosho Tandahimba

Florence Sanawa, Sauti ya Mnyonge, Kanda ya Kusini WAKULIMA Wilayani Tandahimba wameiomba serikali kufanya sensa ya mikorosho ili kuondoa changamoto zilizojitokeza katika msimu wa 2017/18 ambapo wakulima wengi hawakupata pembejeo za bure zilizotolewa na serikali. Akitoa takwimu hizo Mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam Messia Illomo alisema kuwa katika utafiti uliofanywa kwa baadhi ya maeneo wilayani humo ulibaini kuwa katika msimu huu wakulima wametumia gharama kubwa zaidi kuliko misimu yote iliyopita.  “Tulibaini kuwa ni kweli serikali ilitoa pembejeo bure lakini kwa kiasi kikubwa wakulima wamenunua kuliko walizopewa bure pia zilichelewa na zingine zilikuja kwa awamu ya mwisho ambapo ilichelewa sana” “Ujio wa peembejeo kwa awamu kumezua migogoro ya hali ya juu kwa wakulima kwakuwa ilifikia hatua ya kugombana na kufikishana kwenye vyombo vya sheria….. “Lakini pia Bodi ya korosho Tanzania (CBT) iangalie uhahlisia ili kuendana na wakulima wapo wakulima wanasema kuwa pembejeo zili

Mtwara na Lindi mbioni kuingia kwenye gridi ya Taifa

Florence Sanawa, Sauti ya Mnyonge, Kanda ya Kusini Kutokana na kuwepo kwa tatizo kubwa la kukatika kwa umeme katika mikoa ya lindi na mtwara Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imesema kuwa mikoa ya Lindi na Mtwara iko njiani kuingia katika grid ya Taifa ambapo itasaidia kutatua tatizo la umeme lililopo katika mikoa hiyo.   Akizungumza wakati wa ziara yao iliyofanyika jana Mkoani Mtwara Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo Alexander Kyaruzi  alisema kuwa mikoa hiyo itaingia kwenye grid ya taifa baada ya ujenzi wa laini ya kilovoti 400 kutoka mtwara hadi somanga fungu na somanga fungu  hadi kinyerezi kilovote  Alisema kuwa tatizo lililopo hivi sasa linaweza kutatulika kwa kuunganishwa kwenye huo mtambo mkubwa wa umeme ambao ndio unatumiwa na mikoa mingi hapa nchini.   “Hili tatizo la uemme litaisha wakiingia kwenye grid ya taifa ambapo mtambo mmoja utakuwepo Mtwara na mwingine utakuwepo somanga fungu hili ndio litakuwa suluhisho kwa mikoa ya lindi na

Wananchi wadai kuvamiwa na Askari wakimsaka alietoroka chuo cha Mafunzo

WANANCHI wa kijiji cha Kwamgogo shehia ya Mkungu wilaya ya Mkoani, akiwemo mzee wa miaka 55, walijikuta katika mazingira ya taharuki, baada ya kudai kuvamiwa na Askari wa Chuo cha Mafunzo kambi ya Kengeja, muda mfupi baada ya kudai kutorokewa na mwanafunzi wa chuo hicho. Wananchi hao walisema, kati ya Disemba 18 na 19 ya nyakati tofauti, walivamiwa na wapigaji hao wapatao 15 wakiwa na silaha kwa kuanza msako wa nyumba kadhaa hadi kwenye dari, ili kujiridhisha iwapo mwanafunzi wao alietoroka, amefichwa na wananchi hao. Wakizungumza na waandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, mwanachi Abass Fumu Omar (55), alisema yeye alipigwa ngumi tatu za mgongo na teke na watu aliodai kuwa ni askari, wakati alipowauliza kwamba kwanini wanamchukua kijana wao wa mtaani. Alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 2:30 usiku, kabla ya yeye kupewa kichapo hicho, aliona kundi kubwa la Askari hao, wakiwa na silaha, huku wakiwa wamemshikilia kijana alietambulika kwa jina la Mwalimu Juma Silima, kwa lengo l

WATOTO WENYE ULEMAVU WA AKILI MTWARA WASHIRIKISHWE KATIKA MICHEZO

Image
Watoto wenye ulemavu wanapaswa kupewa kipaumbele katika michezo ili kuweza kufanikisha adhima ya kuwajenga kiakilia na kuwafanya wawe na uelewa zaidi katika mambo mbalimbali. Uelewa huo huwafanya wafahamu mambo mbalimbali hali ambayo huchangia kuwaweka karibu na jamii isiyo na ulemavu hivyo kupata uelewa zaidi hasa wanapo changamana.  Watoto hao ambao hushiriki michezo mbalimbali katika na fanikisha kufika katika ngazi ya kitaifa wamekuwa na hali na mori ya kutaka kujua vitu vingi ili waweze kushiriki kikamilifu na wenzao wasio na ulemavu katika michezo ikiwemo kukimbia, kuruka kamba na michezo mingine mingi.  Afisa elimu maalum manispaa ya mtwara mikindani Ally Ndale  anasema kuwa watoto wenye ulemavu wa akili wanapaswa kushirikishwa katika michezo mbalimbali ili kuwachangamsha na jenga. “Watoto wenye ulemavu wa akili huwa wanajifunza taratibu sana ndio maana tunawafundisha kwa njia ya Michezo hii inawajenga kiakili ili kuwaweka katika mazinginra mazuri na kuangalia uwezo wao kiakili

WANYONGE 3,647 NANYUMBU WANUFAIKA BWAWA LA MAJI SENGENYA

Image
WAKAZI zaidi ya 3,647 wa vijiji vinne vya Sengenya, Mara, Matimbeni na Ngalinje Wilayani Nanyumbu Mkoani Mtwara wamenufaika na huduma ya maji safi na salama kutoka katika bwawa la kuvunia maji lilitengenezwa na Halmashauri hiyo kutokana na shida kubwa ya maji iliyopo Wilayani humo. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu Hamis Damumbaya anasema kuwa ubunifu wa mradi huo ulitokana na uhaba mkuwa wa maji unaikabili Halmashauri hiyo.   “ Tunapoendelea kuongeza miradi kama hii ambayo inasimamiwa na jamii yenyewe mbali na kutatua tatizo la maji pia inatatua tatizo la ajira kwa vijana wanaosimamia na kuuza maji hayo hadi sasa kuna maeneo 16 yanayotoa maji moja kwa moja utaona vijana idadi hiyo pia wametapa ajira…… “Unajua serikali imetutaka kuwashirikiana na wananchi pindi wanapoibua miradi kama hii inapokamilika tunawaachia wenyewe waendeshe  hata katika ulinzi wa miundombinu hiyo wamekuwa mstari wa mbele kulinda ikiwemo kulinda mazingira ya bwawa hilo ambalo limekuwa likiw