Posts

Wazazi watakiwa kufichua watoto wenye maradhi ya moyo

Image
Na, Haji Nassor Sauti ya Mnyonge, Pemba WAZAZI na walezi wa watoto wenye maradhi ya moyo Zanzibar, wametakiwa kuwafichua watoto wao, na kuwapeleka katika kliniki za hospotali za serikali, ili kufanyiwa uchunguuzi na kisha kupatiwa matibabu ya haraka. Ushauri huo umetolewa na aliekuwa mgonjwa wa mwanzo Zanzibar kufanyiwa operesheni mbili ndani ya mwezi mmoja nchini Is-rail mwaka 1999  Arafa Abdulla Ali alipokua akizungumza na mwandishi wa habari hizi kisiwani Pemba. Alisema ugonjwa wa moyo unatibika na unapona na kurudi katika hali ya kawaida, hivyo hakuna sababu kwa wazazi au walezi kuwavundika ndani watoto wao. Alisema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia wizara yake ya Afya, imekuwa na ushirikiano mzuri wa kimatibabu na nchi za India na Is-rail, hivyo kwa sasa wazazi hawana sababu ya kuogopa gharama za matibabu, kwa vile hilo hubebwa na nchi husika. Alieleza kuwa, yeye alifanikiwa kupona maradhi hayo ya moyo kutokana na wazazi wake, kumfikisha mapema hospitali ya Mnazi mmoja, na

Mtuhumiwa wa kosa la ubakaji aachiwa huru

Image
Na, Mwandishi Wetu, Sauti ya Mnyonge, Zanzibar BAADA ya kusota rumande kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwili , hatimaye kijana Njile Masalu  Nchilu mkaazi wa Kifumbikai Wete , ameachiwa huru na mahakama ya mkoa wa Kaskazini Pemba. Kijana huyo aliyekuwa anatuhumiwa kwa kosa la kubaka ameachiwa huru na mahakama hiyo baada ya shahidi namba moja ambaye ndiye mwathirika wa tukio hilo kukana kufanyiwa kitendo hicho . Msichana huyo mwenye umri wa miaka 15 , amekana kufanyiwa kitendo hicho mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Makame Mshamba Simgeni na mwendesha mashtaka wa serikali Ramadhan Suleiman Ramadhan , jambo ambalo limeifanya mahakama kuliondoa shauri hilo mahakamani hapo . Baada ya mahakama kuliondoa shauri hilo , kijana Njile aliondoka nduki kali katika viwanja wa mahakama , mithili ya wakimbiaji wa mbio za relay , huku akiwa haamini kilichotokea. Njile alikuwa anakabiliwa na tuhuma ya kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 15 , kosa ambalo alidaiwa kwamba amelitekeleza septemba 5 mwaka 2

Wananchi Pemba walia uchakavu wa barabara

Image
Na, Haji Nassor, Sauti ya Mnyonge, Zanzibar WANANCHI wanaotumia barabara za Wambaa, Kengeja, Kangani, Tundauwa, Chambani na Pujini mkoa wa kusini Pemba, wameiomba wizara husika kuangalia uwezekano wa kuzifanyia matengenezo ya haraka barabara hizo, kabla jazijaongezeka mashimo makubwa. Walisema kwa sasa barabara hizo, zimeshaanza mashimo yenye ukubwa tofauti jambo ambalo huwapa usumbufu wakati wanapozitumia kwa shughuli zao mbali mbali. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti walisema, ni vyema kwa wizara hiyo kuwahi mapema kabla kuharibika zaidi kwa mvua zinazoendelea kunyesha. Walisema baada ya barabara hizo kutumika zaidi ya miaka saba sasa, wakati umefika wa kuzifanyia matengenezo kwa kuziba viraka haraka kabla ya kuchakaa zaidi. Mmoja katia ya wananchi hao Hassan Makame Omar wa Mwambe, alisema sasa barabara yao imeanza kurudi kwenye ubovu wa uwasili wake kutokana na kuzidiwa na mashimo. “Mashimo yameanza kuwa mingi, jambo ambalo hupata mtikisiko mkubwa wanapoku

Afariki dunia kwa kujinyonga akiwa msikitini

Image
Na, Haji Nassor, Sauti ya Mnyonge Zanzibar KIJANA mmoja  Azani Abdalla Suleiman (28)mkaazi wa Ole Mchanga Mrima Mkoa wa Kaskazini Pemba, amefariki dunia usiku wa kuamkia jana, kwa kujinyonga katika Msikiti ulipo kijiji cha Machomane Wilaya ya Chakechake mkoa wa Kusini Pemba. Akithitisha kutokea kwa tukio hilo, kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa kusini Pemba Sheihan Mohamed Sheihan alisema, tukio hilo limegundulika wakati waumini wa dini ya kiislamu, walipofika msikitini kwa ajili ya kusali sala ya alfajiri. Alieleza kuwa mara baada ya watu hao kuingia Msikitini kwa ajili ya kutekeleza ibada hiyo, ndipo walipokutana na mkasa huo na kuona maiti ya kijana huyo ikiwa inaninginia kutokana na kamba aliojifunga. Sheihan alisema taarifa walizobaini kwa haraka sana ni kwamba juzi kijana huyo alifika kwa Babu yake ambae ni Omar Hamad Bakari mkaazi wa Machomane Chake Chake na kumpatia taarifa juu ya adhama yake ya kutaka kufunga ndoa. ‘’Tumeambiwa kwamba hakukua na mafahamiano mazuri na babu yake

Waomba gharama za ‘passport’ kufutwa kwa wagonjwa wa moyo

Image
Na, Haji Nassor, Sauti ya Mnyonge, Zanzibar JUMUIYA ya watoto wenye maradhi ya moyo Zanzibar ‘OCHZ’ imesema, wakati umefika kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar, kukubalia ili kuondoa gharama za hati ya kusafiria “pass port” kwa wagonjwa wa moyo, kwa lengo la kuepusha kukosa kufanyiwa matibabu nje ya nchi, baada ya wafadhili kukubali kugharimia matibabu yao. Mwenyekiti wa Jumuia hiyo dk Omar Mohamed Suleiman, alisema wakati mwengine wagonjwa hao wengi wao wakiwa watoto, hupata ufadhili kutoka kwa mashirika mbali mbali ya kimataifa na watu binafsi, ingawa wapo waliokwama kwa kutokuwa na gharama za pasi ya kusafiria. Akizungumza kwenye mkutano wa siku moja kwa madaktari, wadau wa maradhi ya moyo na wanahabari uliofanyika hospitali ya Chakechake, Mwenyekiti huyo alisema, gharama ya pasi ya kusafiria imekuwa ikiwakwaza, baadhi ya wazazi wenye kipato cha chini, ingawa wakati mwengine huwa wameshapa ufadhili wa matibabu hayo. Alieleza kuwa kupitia Jumuia hiyo, w

Matukio mbalimbali ziara ya Jaji Mkuu wa Zanzibar kisiwani Pemba

Image
JAJI Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, akiangalia kwenye kabati la mahakama ya Mwanzo Chakechake, wakati alipofika kuangali utendaji wao wa kazi, kabla ya kumaliza ziara yake ya siku nne kisiwani Pemba ambapo pia alizungumza na wafanyakazi wa mahakama hiyo WAFANYAKAZI wa Mahakama ya ardhi mkoa wa kusini Pemba, pamoja na mahakama nyengine, wakimsiliza Jaji mkuu Zanzibar Omar Othman Makungu, akizungumza nao kwa nyakati tofauti, kwenye mikutano yake ya ndani, ikiwa ni ziara yake kwenye mahakama hizo, kisiwani Pemba JAJI mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu akiwa na hakimu dhamana wa mahakama ya mwanzo Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, ambapo Jaji huyo alifika mahakamani hapo kuitembelea mahakama hiyo na kuzungumza na wafanyakazi wa mahakama hiyo MRAJI wa Jimbo Mahakama kuu Pemba Hussien Makame Hussien, akizungumza ndani ya Mahakama ya wilaya Konde, mbele ya Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, wakati Jaji huyo akizungumza na wafanyakazi wa Mahakama hiyo Picha zote na Haji Nassor,

TCRA watoa somo la matumizi ya mitandao mkoani Mtwara

Image
Na Sijawa Omary,  Sauti ya Mnyonge, Mtwara WANANCHI katika halmashauri ya wilaya ya mtwara mkoani hapa wameipongeza mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa jitihada zake hasa utoaji wa elimu kwa wananchi hao juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya simu kutokana na kuwepo kwa baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo katika huduma hiyo. Elimu hiyo imetolewa hivi karibuni mjini mtwara na mamlaka hiyo huku waandaji wa mafunzo wakiwa ni shirika lisilokuwa la kiserikali mkoani hapa (MSOAPO) lengo likiwa kuwajengea uelewa zaidi wakazi hao ili waweze kuepukana na changamoto na kuelewa matumizi sahihi ya mitandao mbalimbali ya kijamii kupitia simu zao. Mafunzo hayo yametolewa kwa viongozi kutoka serikali za mitaa katika kata tano kwenye halmashauri hiyo na kwamba wakawe mabalozi wazuri wa kufikisha elimu hiyo ngazi ya chini lakini pia kuhakikisha wananchi wao wanakuwa na uelewa juu ya elimu hiyo. Katika washiriki hao Salum Athumani amesema, elimu hiyo imekuwa na tija kutokana wamekuwa wakikumba